Mfanyabiashara maarufu kutoka nchini Marekani Kylie Jenner ameweka wazi kuwa hakuna tofauti kati yake na dada yake Kim Kardashian kufuatiwa na kuwepo kwa uvumi unaoendelea kuwa wawili hao wapo kwenye mgogoro.
Akizungumza kwenye Keeping up with Kardashians, Kylie Jenner amesema kuwa licha ya makampuni yao ya biashara za urembo na vipodozi yapo tofauti, haimaanishi kuwa hata wao pia wapo tofauti.
Pia Jenner ametoa sifa kwa dada yake na kampuni yake ya KKW Beauty alipokuwa akiongelea jinsi wanavyosaidiana katika kupeana ushauri kuhusu biashara pamoja.
TRENDING STORI
- Babalevo atangaza vita kwa yeyote atakayemtukana Diamond
- Masaa 36 ya mfungwa namba 8612- Doug Korpi
- Samatta ajiunga na Fenerbahce, Aston Villa FC yashuka followers
- Tanzania: Panya anayeweza kugundua mabomu yaliyotegwa ardhini, atuzwa
- Swizz Beatz afunguka sababu za Diamond kuimba Kiduchu kwenye Wasted Energy
“Kim anaweza kutumia urembo wangu nami nikatumia wake, lakiini linapokuja suala la kampuni hapo ndipo tunapoachana, -japo bado tunakuwa pamoja katika kupeana ushauri” amesema Kylie.

Kylie pia amezungumza kuhusu familia yao, ushirikiano wao na dada zake wengine ambao ni Kourtney Kardashian 41, Khloe Kardashian 36, Rob Kardashian 33, na Kendall Jenner 24, amefunguka kuwa bado wana upendo katikati yao na wote hukumbushana juu ya baraka walizonazo



Categories: BURUDANI
1 reply »